Home
 About UNIC
 Media Accreditation
 Latest News
 UN Gazeti
 Library and Publications
 UN Days & Observances
 UN in Kenya Person of the year
 Model United Nations
 Educational Outreach
 Liaison with NGOs
 UNIC Nairobi Photo Gallery
 Key UN Resources
 UN Agencies in Nairobi
 UN Agencies in Kampala
 UN Agencies in Victoria
 
Depository Libraries
University of Nairobi
Moi University
Makerere University
 
Other Resources
Online Databases
UNBISNET Database
UN Sales Publications
Publications in Kiswahili

Kiswahili Publications

Umoja wa Mataifa - Haki za Binadamu

UTANGULIZI

Kwa kuwa kukiri heshima ya asili na haki sawa kwa binadamu wote ndio msingi wa uhuru, haki na amani duniani, Kwa kuwa kutojali na kudharau haki za binadamu kumeletea vitendo vya kishenzi ambavyo vimeharibu dhamiri ya binadamu na kwa sababu taarifa ya ulimwengu ambayo itawafanya binadamu wafurahie uhuru wao wa kusema, kusadiki na wa kutoogopa cho chote imekwisha kutangazwa kwamba ndio hamu kuu ya watu wote, Kwa kuwa ni lazima, ili mtu asishurutizwe kuomba msaada kutokana na maasi ya kupinga dhuluma na uonevu, kwamba haki za binadamu ziwe chini ya ulinzi wa sheria, Kwa kuwa ni lazima kabisa kuendeleza uhusiano wa kirafiki kati ya mataifa, Kwa kuwa watu wa Umoja wa Mataifa wamethibitisha tena katika Mkataba wao imani yao katika haki za asili, heshima na thamani ya binadamu na katika usawa wa haki kwa wanaume na wanawake, na kwa sababu wamekata shauri la kuendeleza mambo ya starehe na hali bora za maisha ya watu kwa kuwa na uhuru zaidi, Kwa kuwa Nchi zilizo Wanachama zimeahidi, kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa, kukuza na kuheshimu haki za binadamu na uhuru wake wa asili, Kwa kuwa kuzitambua haki hizi na uhuru huu ni jambo la maana sana kua kutimiza ahadi hiyo, Kwa hiyo basi, BARAZA KUU linatangaza TAARIFA HII YA ULIMWENGU JUU YA HAKI ZA BINADAMU kama ndio nguzo ya juhudi kwa watu wa mataifa yote ambayo hatimaye kila mtu na kila jamii ya watu - kwa kushikilia daima Taarifa hiyo - watajitahidi kufundisha jinsi ya kukuza heshima ya haki hizo na uhuru huo. Na mataifa yote yatajitahidi kuzifanya haki hizo zifahamike miongoni mwa Nchi zilizo Wanachama na miongoni mwa watu zinaowatawala.

Jalida zilizoandikwa kwa Kiswahili